Mwili wa Mwanaume Uliokatwa Kichwa Wapatikana Ukielea Mtoni Kisumu
Na : Mweru Mbugua
Polisi wa Kisumu wameanzisha operesheni ya kuutoa mtoni mwili wa mwanaume aliyekutwa ukiwa umekatwa kichwa, ukielea katika mto uliopo eneo la Chemelil
Kwa mujibu wa ripoti ya polisi, mwili huo uligunduliwa Jumanne na wanaume wawili waliokuwa wakivua samaki kando ya mto
Mwili huo ulikuwa umeanza kuoza na ulikuwa umefungwa ndani ya gunia la kijani, hali iliyozua shaka ya kuwepo kwa mauaji

Maafisa wa polisi waliofika eneo la tukio walithibitisha kuwa mwili huo haukuwa na kichwa
Hata hivyo, juhudi za kuutoa mtoni hazikufanikiwa kutokana na giza na kina kirefu cha mto
Operesheni hiyo ilisimamishwa na inatarajiwa kuendelea tena leo asubuhi, huku maafisa wa idara ya uchunguzi wa matukio kutoka Kisumu wakitarajiwa kujiunga na juhudi hizo kadri uchunguzi unavyoendelea




